Wananchi wa Kijiji cha Lyowa kata ya Muungano Wilaya na Mkoa wa Mtwara wamefunga Shule ya Msingi ya Kijiji hicho, Wamefunga Ofisi ya Mtendaji wa Kijiji, Wamemlazimisha Mwenyekiti wa Kijiji kujiengua katika nafasi hiyo lakini pia zaidi ya Wanachama 200 wa Chama cha Mapinduzi CCM wamerudisha Kadi za Chama hicho wakishinikiza kupewa pesa za Mama Samia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Milioni 560 kwa ajili ya ukamilishaji wa Shule yao ya Sekondari,.
Faida Online TV tumefika Kijijini hapo na kuzungumza na Wananchi hao, Mwenyekiti aliyelazimishwa kujiweka kando, Pamoja na Mh. Diwani wa Kata hiyo na Baadae kubisha hodi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Mh. Hanafi Msabaha.
SUBSCRIBE YOTUBE CHANNEL YA FAIDA ONLINE TV ILI KUPATA HABARI ZETU.